Saturday, June 29, 2013

ASKARI POLISI WAJIPANGA KUHARIBU BIASHARA YA MAKAHABA WAKATI WA ZIARA YA RAIS WA MAREKANI BARACK OBAMA.




https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjF8-Tj7wX3GADEFSYm8mSJCgzf7UqPbfbBtpYZQnfh5JmiMxerWomXVoT5kjbh3hfqKGUZizPebB_y9TphQ7z6sqoqSBAyUMSmD9aASVixhTlv9rdmsctMP1pQwHiAge_gC1zTHAHubcc/s640/47284_548071621874168_1124142634_n.jpgWAKATI  wafanyabiasha ya ukahaba jijini Dar es Salaam wakijipanga kutekeleza kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe, yakuwataka watanzania kuchangamkia  biashara zao na kutokubali wageni warudi na  dola makwao, Jeshi la polisi limejipanga kuwadhibiti.

WAKATI  wafanyabiasha ya ukahaba jijini Dar es Salaam wakijipanga kutekeleza kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe, yakuwataka watanzania kuchangamkia  biashara zao na kutokubali wageni warudi na  dola makwao, Jeshi la polisi limejipanga kuwadhibiti.

Wakizungumza na habarimpya.com makahaba hao waliokuwa wamejipanga kujipatia pesa za kigeni kutoka kwa baadhi ya wageni ambao wangewahitaji, walisema Askari Polisi wamejipanga kuvuruga biashara zao.  

Hatua ya Jeshi la Polisi kuendelea kuwasaka makahaba hao imezidi kuvuruga mipango yao ya kupata dola chap chap, oparesheni ina yozidi kufanyika hasa maeneo ya Kinondoni, pengine ikabunguza dola chap chap kama alivyo agiza Membe.

“Kwa kweli mpaka sasa hatujaelewa itakuwa vipi kwani ni kitu cha ajabu sana  na imekuwa tofauti  na matarajio tuliyokuwa tumejiwekea,mwanzoni tuliifurahia sana kauli ya waziri Membe iliyosema,watanzania tuchangamkie biashara zetu, tusizubae wageni warudi na dola zao kwao sasa naona imekuwa kinyume kwani ulinzi uliopo ni balaa” alisema mmoja wa makahaba aliyejitambulisha kwa jina la Zamda aliyesafiri kutoka Dodoma kuja jijini Dar es Salaam.

Mbali na Makahaba, wamachinga pia wameonekana kukosa maeneo ya kufanyia biashara zao katika maeneo mabalimbali ya jiji, baada ya Polisi kuongoza oparesheni hiyo inayoendelea  sehemu mbalimbali za jiji hilo.

Akizungumza na Habarimpya.com Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni Camillus Wambura  alisema, “Tumeamua kuimarisha ulinzi wa Jiji na kuliweka safi jiji letu, sio kwa ajili ya ujio wa Rais Obama tu, bali  hii  oparesheni mpya itakayo endelea kufanyika ndani ya jiji hili hata wageni hawa pindi watakapo ondoka, tumeamua kuifanya Kinondoni kuwa mpya kwa kuzuia mambo yote yanayotendeka kinyume cha  sheria”.

ONA SASA

ONA SASA

Leo jioni wakati natoka katika shughuli zangu nilipita maeneo ya Mwenge pale stand ya mabasi nimekuta kweupe wale vijana wanao uza nguo kwa kupanga chini na kuzishika sikuwaona ...nikauliza nikaambiwa wamefukuzwa kwa ajili Oboma Anakuja...Mmhhh Kazi kweli kweli.

Wakati bado nashangaa shangaa Mara lik
aja gari la Polisi na Wale mgambo wa jiji...Mara nikaona watu wanakimbia huku na kule.

Kushangaa kumbe wale wamachinga bado wapo ila wanauza kwa kujificha ficha kwenye vichochoro vya maduka..Sasa Kimbembe kikaanza wale wanamgambo wakawafuata huko huko na kuanza kuwapiga na kuwavunjia meza na viti vyao.

Kwa kweli iliniuma sana kuona watanzania wenzetu wakifanyiwa hivyo ....Bado sijapata jibu ...siko zote mbona hawakufukuzwa ?? Huu Ugeni ndio imekuwa Nogwaaaaa.

Na uhakika kuna ambao wanalisha na kutunza familia kwa kazi hizi za umachinga sasa watakula wapi kama hali ndio hiyo. ?
Serikali yetu haiwajali watu wake bali inawathamini wagani